Friday, May 1, 2015

DALILI 5 ZA MWENZA BORA WA NDOA

Ni kweli kuwa karibu vitabu vyote vya dini vinasisitiza kuwa na mwenza wa maisha kama njia sahihi ya kuishi maisha yako ya kimapenzi na pia kutimiza majukumu mengine ya kuendelezana kati ya jinsia hizo mbili. Katika makala hii mambo ya msingi ya kuepuka ili upate mke atakayekidhi maelekezo ya vitabu vya dini, yaani mke bora. Kabla ya kuenda mbali tujikumbushe vitabu vinasema nini kuhusu mke bora:
"Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao fikiri."--Qur'an 30:21 http://www.theholyquran.org/
Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana. 
-         Mithali 18:22 https://www.wordproject.org
Sintokuchosha na mistari mingi toka vitabu vya dini, hiyo miwili hapo juu inatosha kueleza ubora na umuhimu wa kupata mwenza sahihi wa ndoa. Hata hivyo swali gumu linalowakwamisha wengi ni kuwa je unamjua mwanamke atakayeweza kuwa mke mwema ?

Usitegemee kumrekebisha wakati mmeshaoana: 
Ndoa sio uwanja au shule ya mafunzo kwa mke wako kuishi unavyotaka hivyo usitegemee kuoa mke mwenye tabia fulani usizozipenda kwa kujipa moyo akiwa katika ndoa atajirekebisha. Je asipojirekebisha ? Hapo ndo mwanzo wa migogoro isiyoisha.Unamkubali mke maana yake umemchunguza na kusema “namkubali” , na kama kuna madhaifu basi maana yake umekubali kuishi nayo kwani hata wewe pia una madhaifu yako.

Anaonyesha vitendo sio tuu maneno: 
Ni zaidi ya kuwa mcha Mungu kwa maana ya muonekano wa kuenda msikitini au kanisani, bali anaonyesha vitendo kuwa ni mwenye huruma, mpole kiasi, na mwenye kuthamini wengine.

Sio mfuata upepo:  
Mke bora ana uhuru wa fikra sio tuu dhidi ya wewe kukubaliana na kila jambo unalotaka , ila pia anakuwa na uwezo wa kuchambua anayoyasikia toka nje ya ndoa yenu na kubaki na mtazamo chanya wa mahusiano yenu. Hata kwa wewe mwenyewe hatokuwa mfuata upepo wa kila utakacho kwani kumbuka kuwa yeyé ni msaidizi wako, hivyo kuwa tayari pale atakapokurekebisha na kukukosoa .

Mdadisi na mwenye kujifunza
Nyote mnapoanza mahusiano mnakuwa na ndoto ya maisha ya furaha na mafanikio. Hata hivyo kadri siku zinavyoenda na mabadiliko ya kijamii, kiuchumi, na nyie wenyewe pia mnabadilika kitafakari  na kimahitaji. Mke bora atapenda kuwa mdadisi na kujifunza kukabiliana na mabadiliko haya ili kuendelea kutunza ndoa yake.


Mmejadili naye mambo ya msingi kuhusu maisha yenu ya baadae na unafahamu msimamo wake
Katika makala yetu ya  siku za nyuma tulijadili  kuwa kuna mambo 6 yanayoweza kuhatarisha mahusiano yenu kama hamtojadili na kufikia muafaka. Mambo hayo ni fedha, imani, mahala pa kuishi, watoto, falsafa ya maisha na  hisia za mapenzi. Soma zaidi BOFYA HAPA

0 comments:

Post a Comment