Iwe unatafuta msaada wa kifedha, ushauri au ushirikiano katika
lile unalolifanya ni vema ukatambua namna bora ya kuelezea unalolihitaji kwa
mtu au taasisi husika. Pia haitoshi kujieleza unahitaji nini, inakupasa uwe mtu
ambaye kweli unastahili kusaidiwa.
Yafuatayo ni baadhi ya mambo yanayokwamisha wengi katika kuomba msaada:
Kushindwa kujieleza kwa ufasaha
Wewe ndie unayejua haswa
unachohitaji, hivyo inakupasa kufafanua kile unachokifanya, wapi umekwama, na
nini unahitaji huyo mtu mwingine afanye, na afanye kwa kiwango gani, na kwanini
akusaidie wewe. Mfano mara
nyingi nimepokea meseji mtu ananiambia “Bro naomba nitafutie schorlaship”. Hili si ombi lililojitosheleza kwani ,
schorlaship ni swala pana, ni schorlaship ya nini, wapi, kwanini unastahili
kupata schorlaship n.k. Kama wewe unayeomba unashindwa kutumia muda wa kutosha
kufafanua unalohitaji, kwanini mtu mwingine atumie muda wake kujadiliana nawe
ili ajue haswa unachohitaji. Ni muhimu kuonyesha kweli una juhudi katika hicho
unachokitafuta.
Kutokuwa na
mahusiano mazuri
Mara nyingi mtu
anayeweza kukusaidia ni yule anayekuthamini na kukufahamu. Mtu hawezi
kukusaidia kama taswira yako kwake ni mtu usiyeaminika, usiyejitambua na
usiyemheshimu na kumjali au kujali wengine. Ni vizuri basi kuwa na mahusiano
mazuri na huyo unayetarajia kuomba msaada kwake, na pia ujenge taswira nzuri
kwa jamii kwa kufanya mambo ya msingi.
Kutokutoa
mrejesho
Unapopata msaada kumbuka kwanini mtu huyo alikusaidia kwa mara ya
kwanza. Sio tuu kwakuwa uliomba, ila amini mtu huyo anahitaji kujua tokeo la
msaada wake. Wengi wanaposaidiwa huacha kueleza matokeo ya msaada waliopewa.
Kutotumia
vizuri msaada
Ulimuanisha mtu aliyekupa
msaada ulikuwa kweli mwenye kuhitaji huo msaada ndio maana ukapewa, hata hivyo
kidogo ulichosaidiwa umeenda kitumia tofauti. Kwanini huyo mtu awe na imani
akikusaidia tena, msaada wake utaenda kutumika ipasavyo.
Kutokuonyesha
wanastahili kusaidiwa
Kwa mtu anayeweza
kukusaidia kwake ni muhimu kujua kama kweli unastahili kupokea huo msaada wake
kwani si unajua hiyo ni mali iwe ni muda wa kukushauri au ni pesa za kufanyia
biashara au shule. Sidhani kama mtu unayemuomba msaada anawaza kupoteza tuu
msaada wake. Na njia ya yeyé kujua kama hatopoteza msaada wake ni kujua kuwa
wewe unastahili kusaidiwa. Vitu anavyoweza kuangalia ili kujua kama unastahili
kusaidiwa ni pamoja na uaminifu , ujuzi, uzoefu wako, taswira yako , mahusiano yake na yeye, n.k
Kuogopa
kuomba msaada
Kuna baadhi ya watu huogopa kujitokeza kuomba msaada, kwa sababu
mbalimbali ikiwemo kutojiamini, kuogopa au kushindwa kujieleza, na wakati
mwingine hata kutokuamini kama wanaweza kusaidiwa.
HITIMISHO:
Je, wewe ni miongoni mwa wenye matatizo yaliyotajwa hapo juu ? Tuzungumze tuone
tunalitatuaje tatizo hilo. Like ukurasa wetu wa Facebook, na unitumie meseji.
0 comments:
Post a Comment